"

SURA YA V: SHUGHULI ZA KILA SIKU

21 Lesson 2: Ratiba Yangu

Performance Objectives

By the end of this lesson, the learner will be  able to:
  • describe what you do regularly
  • master telling time
  • give their daily schedule using the habitual hu-

Msamiati wa shughuli za kila siku

Kiswahili English Kiswahili English
Kuamka To wake up Kuoga To shower
Kulala To sleep Kuimba To sing
Kucheza To play Kula chakula cha asubuhi To eat breakfast
Kutazama televisheni To watch TV Kula chakula cha jioni To eat dinner
Kusikiliza muziki To listen to music Kutembeza mbwa To walk the dog
Kulala To sleep Kusafisha vyombo To clean dishes
Kuenda shuleni To go to school Kupika chakula To cook food
Kusoma To read/to study Kupiga huva To vacuum
Kupiga mwaski To brush teeth Kuosha bafu na choo To clean the toilet and the bathroom
Kunawa uso To wash the face Kucheza dansi To dance
Kucheza muziki To play music Kusafiri To travel
Kula chakula cha mchana To eat lunch Kwenda shuleni To go to school
Kwenda kazini To go to work Kwenda darasani To go to class
Kulima shamba To till the land Kufagia To sweep
Kukama ng’ombe To milk a cow Kupiga deki To mop
Kukata nyasi To cut grass/mow the lawn Kutandika kitanda Make bed

Zoezi la 1: Msamiati

These activities are common among family and friends in East Africa. In groups of 3, compare and contrast and mark activities that are shared between East Africans and your own culture.

Watu hufanya nini? Mwanafunzi 1 Mwanafunzi 2 Mwanafunzi  3
Kusikiliza muziki
Kukama ng’ombe
Kupika chakula
Kukata nyasi
Kwenda kazini
Kula chakula cha asubuhi
Kwenda shuleni
Kufagia
Kucheza dansi
Kulima shamba
Kuoga
Kulala
Kuosha bafu na choo
Kutandika kitanda
Kupiga deki

Discuss the similarities and differences between your own cultures and the East African culture.

 

Zoezi la 2: Kusoma

Monolojia 1: Ratiba ya Juma

Mimi ni Amina. Mimi huamka saa moja kamili asubuhi. Baada ya kuamka mimi huoga kisha hupiga mswaki. Baada ya kupiga mswaki mimi huvaa nguo kisha hupika chakula cha asubuhi. Mimi hula chakula cha asubuhi saa mbili kamili. Mimi huenda darasa la Kiswahili saa nne na dakika kumi asubuhi hadi saa tano kamili mchana. Baada ya darasa la Kiswahili mimi huenda darasa la Kemia kisha mimi hula chakula cha mchana saa sita kamili mchana. Kisha mimi huenda nyumbani.

Maswali (Write all times in numbers)

  1. Jina lake ni nani?
  2. Amina huamka saa ngapi?
  3. Amina hufanya nini baada ya kuamka?
  4. Yeye hufanya nini kabla ya kupika chakula cha asubuhi?
  5. Amina huenda darasa la Kiswahili saa ngapi?
  6. Darasa la Kiswahili huisha saa ngapi?
  7. Yeye hula chakula cha mchana saa ngapi?

Zoezi la 3: Ratiba ya Imani ya Asubuhi (KUSIKILIZA)

Write a summary of Imani’s schedule below

Zoezi la 4: Kueleza ratiba yako

  • You and your friend are trying to find a time to meet on Monday to work on a class project. You decide to send her a quick summary of your Monday schedule to help coordinate.

Zoezi la 5: Andika sentensi kueleza ratiba ya Jamila

Based on the pictures provided, write six sentences to describe Jamila’s evening schedule.

Photo by Greg Pappas on Unsplash

Photo by Kevin McCutcheon on Unsplash

Photo by Kevin McCutcheon on Unsplash

Photo by Diana Polekhina on Unsplash

Photo by Jingxi Lau on Unsplash

Photo by Alexunder Hess on Unsplash

Zoezi la 6: Kusoma

Soma kuhusu ratiba ya Malaika kisha ujibu maswali. (Malaika describes her schedule to Jamila and Amina. They are trying to figure out a time to meet for brunch, lunch, or dinner, but Malaika’s day seems to be busy.

Hamjambo rafiki,

Mimi huwana kazi na madarasa mengi kila siku. Mimi huamka saa mbili na nusu asubuhi. Baada ya kuamka, mimi huoga, huvaa nguo, na hupiga mswaki. Kisha mimi hupika chakula cha mchana. Mimi hupakia na kubeba chakula cha mchana. Mimi huwa sili chakula cha asubuhi. Mimi huenda darasani saa tatu kamili asubuhi hadi saa tatu na dakika hamsini mchana. Baada ya darasa mimi huenda kazini kutoka saa nne kamili mchana hadi saa sita na nusu mchana. Baada ya kazi mimi hula chakula cha mchana kisha huenda darasa la Biashara saa saba kamili hadi saa nane na dakika ishirini. Baada ya darasa mimi hupumzika kisha hufanya mazoezi kutoka saa tisa na nusu hadi saa kumi na nusu. Mimi huenda darasa la Anthropolojia saa kumi na moja kamili hadi saa kumi na mbili na dakika ishirini. Mimi huenda nyumbani saa kumi na mbili na nusu.

Asanteni,

Malaika

Maswali

  1. Malaika huamka saa ngapi?
  2. Malaika hufanya nini baada ya kuamka?
  3. Malaika huenda darasa la kwanza saa ngapi?
  4. Malaika huenda darasa la mwisho saa ngapi?
  5. Malaika huanza kazi saa ngapi?
  6. Malaika hufanya nini kabla ya Kwenda darasa la Athropolojia?
  7. Malaika hufanya nini baada ya kupika chakula cha mchana?
  8. Malaika hula chakula cha asubuhi saa ngapi?
  9. Malaika huenda nyumbani saa ngapi?
  10. Malaika hupumzika kwa muda gani?

Zoezi la 7: Kuzungumza Ratiba ya Maria

Your friend Maria called you and left a voicemail about an excursion they have over the weekend. They would like to know your schedule so they can plan activities and meals for the excursion. Record a voice note giving your schedule.

License

Icon for the Creative Commons Attribution 4.0 International License

Elementary Swahili I Copyright © by Gorrety Wawire is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License, except where otherwise noted.